Home Makala Senzo Aachia Mikoba Simba

Senzo Aachia Mikoba Simba

by Sports Leo
0 comments

Tetesi zinaeleza kuwa ofisa mtendaji mkuu wa Simba, Senzo Mazingisa siku ya Jana jioni alikabidhi ofisi na nyaraka za klabu hiyo kwa madai ya kuwa hakuwa akisikilizwa huku taarifa zingine zikieleza kuwa mkataba wake umeisha.

Pia  kuna kikao kimeendelea leo ambacho wamejadili kuhusu mbadala wake na nani atakaimu kwa wakati huu huku mchakato mwingine wa kutangaza ajira ukifuata hapo baadaye.

Bodi ya Simba Sc imejadili kuwa mtu atakayepatikana kukaimu nafasi hiyo kutoka ndani ya kikao hicho hapaswi kutoka kwenye bodi ya wakurugenzi  kwa maana kuwa asiwe mjumbe wa bodi hiyo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited