Home Makala Serena ajitoa Wimbledon

Serena ajitoa Wimbledon

by Sports Leo
0 comments

Mwanamama nguli katika mchezo wa tenisi Serena Williams amejiondoa katika mashindano ya Wimbledon baada ya kuumia katika mchezo wa mtoana dhidi ya Aliaksandra Sasnovich.

Williams aliteleza katika set ya tano ya mchezo na ilipofika set ya saba alishindwa kuendelea kutoana na maumivu makali ya nyama za paja’,hali iliyomsababishia kumwaga machozi.

Mashabiki waliohudhuria walimpigia makofi wakati akitoka uwanjani.

banner

Hili linakuwa pigo kubwa kwa Serena anayepambana kuvunja rekodi ya kuwa mchezaji wa tenisi wa kike mwenye mataji mengi  zaidi, ambapo mara kwa mara jaribio lake la kutwaa taji la 20 limekuwa likishindikana.

Serena aliwashukuru mashabiki zake waliokuwa wakimtia moyo kwa sapoti yao.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited