Klabu ya Simba Sc imezidi kujisogeza kileleni mwa msimamo wa ligi kuu ya Nbc nchini baada ya kuifunga timu ya Pamba Jiji Fc kwa mabao 5-1 katika mchezo wa ligi kuu ya Nbc nchini uliofanyika katika uwanja wa Kmc Complex uliopo Mwenge jijini Dar es Salaam.
Pamba jiji Fc hawakutoka hivihivi ambapo Methew Momanyi alifunga bao la kufutia machozi kutokana na uzembe wa mabeki wa Simba sc ambapo aliuchopu vizuri mpira uliomshinda kipa Moussa Camara dakika ya 86 ya mchezo.
Simba sc sasa imefikisha alama 66 katika nafasi ya pili ya msimamo wa ligi kuu ya Nbc huku wakiwa na mchezo mmoja mkononi ambapo Yanga sc anaongoza msimamo wa ligi akiwa na alama 70.