Home Makala Simba Wabeba Taji Ngao Ya Jamii

Simba Wabeba Taji Ngao Ya Jamii

by Dennis Msotwa
0 comments

Simba Sc imefanikiwa kutwaa taji la ngao ya jamii leo kwenye mchezo uliochezwa uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Wanamsimbazi hao wametwaa taji hilo baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 mbele ya Namungo Fc ambapo bao la kwanza lilipachikwa na John Bocco kwa mkwaju wa penalti dakika ya 7 baada ya Morrison kuchezewa faulo ndani ya 18.

Bao la pili lilifungwa na Benard Morrison katika kipindi cha pili cha mchezo dakika ya 59 ambapo ushindi huo ulidumu dakika 90 za mchezo na kuifanya Simba kutwaa taji la ngao ya jamii mbele ya Namungo Fc inayonolewa na Hitimana Thiery.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited