Home Makala Simba Wazitaka Tatu Za JKT

Simba Wazitaka Tatu Za JKT

by Sports Leo
0 comments

Kikosi cha Simba Sc kimesema kuwa kipo tayari kwa ajili ya mchezo wa leo utakaopigwa uwanja wa Jamhuri dhidi ya JKT Tanzania ikiwa ni mchezo wa raundi ya tano ligi kuu bara.

Simba Sc iliyochini ya kocha mkuu Sven Vandernbroeck watakutana na JKT Tanzania majira ya 1:00 usiku ambapo matarajio yao makubwa ni kupata matokeo chanya licha ya muda mrefu kutotumia uwanja huo.

Mchezo huo utakuwa ni wa ushindani mkubwa kwani wote wanazihitaji pointi tatu ikiwa Simba wametoka kulazimisha sare ya kufungana bao 1-1 na Mtibwa Sugar huku JKT Tanzania wakiwa wamefungwa bao 1-0 na Coastal Union.

banner

JKT Tanzania ipo nafasi ya 14 ikiwa na pointi 4 kibindoni inakutana na Simba iliyo nafasi ya 3 na pointi 10.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited