Site icon Sports Leo

Simba Yaahidi Kutolea Ufafanuzi Wa IST Ya Kabwili

Ramadhani Awam Kabwili of Tanzania during the 2017 Under 17 Africa Cup of Nations Finals football match between Mali and Tanzania at the Libreville Stadium in Gabon on 15 May 2017 ©Samuel Shivambu/BackpagePix

Uongozi wa Simba Sc umeahidi leo kutolea ufafanuzi suala la  mlinda mlango wa Yanga Ramadhan Kabwili kudai kuwa aliahidiwa gari aina ya Toyota IST endapo angepewa kadi mbili za njano kweye mchezo wao wa msimu uliopita 2018/19.

Ofisa mkuu wa habari Simba Sc Haji Manara amesema kuwa watajibu tuhuma alizotoa mchezaji huyo ila cha msingi ajiandae kikamilifu na ushahidi wa tuhuma hizo.

Shirikisho la soka Tanzania (TFF) limetoa  taarifa ya kusikitishwa na taarifa hizo kwa kuwa si mpango mzuri kwa maendeleo ya soka na wameahidi kulifanyia uchunguzi kwa kujulisha vyombo vingine vya usalama ili viweze kubaini ukweli na hatua stahiki ziweze kuchukuliwa.

Cliford Ndimbo ambaye ni ofisa habari wa shirikisho la soka Tanzania amesema kuwa TFF siku zote imekuwa ikipiga vita vitendo vya upangaji matokeo katika mpira wa miguu na hivyo wanahidi kulifanyia uchunguzi wa kina swala hili.

Exit mobile version