Home Makala Simchimba Ajifunga Azam Fc Hadi 2023

Simchimba Ajifunga Azam Fc Hadi 2023

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji wa Azam Fc, Andrew Simchimba ambaye alikuwa kwenye hesabu za mabosi wa Simba Sc waliokuwa wanahitaji saini yake msimu wa dirisha dogo na dili lao kutibuliwa amejifunga ndani ya klabu ya Azam kwa kandarasi ya miaka mitatu.

Nyota huyo aliyekuwa anakipiga Coastal Union hapo awali na kurejea Azam Fc mkataba wake ulikuwa umalizike mwaka huu mwezi Septemba lakini ameongezewa kandarasi ya miaka mitatu ambapo atadumu hapo hadi 2023.

Uongozi wa Azam Fc umekuwa unamuamini Simchimba kwani amekuwa akitimiza majukumu yake kwenye timu hiyo kama ipasavyo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited