Home Makala Sita Wasajiliwa Mbao Fc

Sita Wasajiliwa Mbao Fc

by Dennis Msotwa
0 comments

Uongozi wa Mbao Fc wamefanikiwa kufanya usajili wa wachezaji sita katika kipindi cha usajili wa dirisha dogo lililofungwa juzi usiku.

Mwenyekiti wa kikosi hicho Solly Njashi alisema kuwa wamejipanga vyema katika kuhakikisha timu yao inafanya vizuri katika michezo ya ligi kuu  iliyobaki.

Waliosajiliwa kwa mkataba wa miaka miwili ni Hussein Iddi kutoka Mtibwa Sugar Omary Wayne kutoka Friends Rangers na Wilson Wilson.

banner

Mackyanda Franko kutoka Coastal Union kwa mkataba wa miezi sita Hamis Mwinshehe kuttoka JKU ya Zanziabar kwa mkataba wa mwa mmoja na Paulo Maige kutoka Azam Fc kwa mkataba wa miaka mitatu.

Kocha mkuu wa timu hiyo Hemedi Moroco amesema kuwa ana imani kubwa na wachezaji hao watasaidia kuinua kikosi na kukipa nguvu katika michezo ya ligi kuu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited