Home Makala Sowah Atua Singida Black Stars

Sowah Atua Singida Black Stars

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Singida Black Stars imekamilisha usajili wa mshambuliaji raia wa Ghana Jonathan Sowah kwa mkataba wa miaka miwili kutoka klabu ya Al Nasser ya nchini Libya.

Usajili wa mshambuliaji huyo umekamilika baada ya tetesi za muda mrefu kuwa atajiunga na timu hiyo huku pia ikisemekana hata Yanga sc nao walikua wakimzea mate.

banner

Singida Black Stars imemsajili mshambuliaji huyo baada ya kununua mkataba wake kutoka klabu hiyo na anatarajiwa kuungana na Elvis Rupia pamoja na Eliuter Mpepo kuongoza safu ya ushambuliaji klabuni hapo.

Ikiwa imemtambulisha kocha mpya Hamdi Miloud baada ya kuachana na kocha Patrick Aussems na benchi lake lote la ufundi,sasa klabu hiyo imeweka kambi maalumu ya mafunzo ambapo kocha huyo atachomeka mbinu zake kabla ya ligi kuu kurejea februari mosi.

Katika msimamo wa sasa wa ligi kuu nchini Singida ipo nafasi ya nne ikiwa na alama 33 baada ya kucheza 16 ya ligi kuu ya Nbc.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited