Home Makala Sowah Kupishana na Guede Singida Bss

Sowah Kupishana na Guede Singida Bss

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji Jonathan Sowah yupo mbioni kujiunga na timu ya Singida Black Stars akichukua nafasi ya Joseph Guede ambaye amefikia makubaliano ya kuvunja mkataba wake na klabu hiyo.

Sowah ambaye anaichezea Al Ahli Benghaz ya nchini Libya anajiunga na klabu hiyo baada ya timu hizo mbili kufikia makubaliano ya dau la dola 200,000 za kimarekani ambapo ilisemekana kuwa staa huyo atajiunga na Black Stars wakati wa dirisha hili la usajili.

Taarifa kutoka ndani ya Singida Black Stars zinasema kuwa Sowah anakuja kuungana na Elvis Rupia kama washambuliaji kinara wa klabu hiyo ambapo anatarajiwa kupokea mshahara kiasi cha dola elfu tano ambapo atakua moja ya mastaa wanaopokea mshahara mkubwa klabuni hapo.

banner

Mpaka sasa Singida Black Stars ina alama 30 katika ligi kuu ya Nbc nchini ikiwa imecheza jumla ya michezo 14 ya ligi kuu katika nafasi ya pili nyuma ya Azam Fc.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited