Home Makala Stars Yapigwa Chan

Stars Yapigwa Chan

by Dennis Msotwa
0 comments

Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) imepoteza mchezo wa kwanza wa michuano ya kombe la mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani(Chan) baada ya kufungwa mabao 2-0.

Kipindi cha kwanza kilimalizika kwa suluhu hukiu Stars ikijitahidi kuonyesha ubabe kwa kushambulia japo haikupata bao licha ya kulaimisha mashambulizi.

Kipindi cha pili Stars ilikata upepo na kusababisha mabao mawili huku makosa ya Shomari Kapombe yakisababisha bao la kwanza dakika ya 61 baada ya kuunawa mpira ndani ya boksi na mwamuzi kuipa penati Zambia iliyofungwa na Collins Sikombe dakika ya 64.

banner

Uzembe wa mabeki wa Stars ulisababisha Zambia kupata bao la pili dakika ya 81 mfungaji akiwa Emmanuel Chabula aliyeunganisha krosi kwa shuti kali na kufanya dakika tisini kumalizika kwa stars kupoteza alama tatu muhimu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited