Home Makala Tajiri Chelsea Akubali Yaishe

Tajiri Chelsea Akubali Yaishe

by Dennis Msotwa
0 comments

Tajiri wa klabu ya Chelsea Roman Abramovich amekubali kuuzwa kwa klabu ya Chelsea huku Serikali ya Uingereza ikisimamia kila kitu ikiwemo kuchukua faida ya uuzwaji wa timu hiyo inayofanya vizuri nchini humo.

Awali baada ya Urusi Kuivamia Ukraine mataifa ya Nato ambayo Uingereza ni mwanachama yaliiwekea vikwazo vya kiuchumi serikali ya Urusi chini ya Vladimir Putin ikiwemo kuzuia mali zote za matajiri wa kirusi nchini humo ambapo klabu ya Chelsea imeathirika kutokana na mmiliki wake kuwa Mrusi huku akitajwa kuwa rafiki wa karibu wa Putin.

Akaunti za klabu hiyo tayari zimefungwa huku wakiruhusiwa kufanya shughuli chache za soka chini ya usimamizi wa serikali ya Uingereza ambao pia walizuia kuuzwa kwa klabu hiyo lakini uamuzi wa bilionea huyo kuruhusu kukabidhidi usimamizi wa uuzwaji kumilikiwa na serikali imekua ahueni kwa klabu hiyo kuendelea na mchakato wa uuzwaji.

banner

Chelsea ipo katika nafasi ya tatu ya msimamo wa Epl ambapo imepitwa na kinara Man city kwa alama 13 huku ikikazana angalau kumaliza katika nne bora ili kupata kushiriki michuano ya Uefa mwakani.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited