Home Makala TFF Yaunda Kamati Ya Ushindi Taifa Stars

TFF Yaunda Kamati Ya Ushindi Taifa Stars

by Dennis Msotwa
0 comments

Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Wallace Karia, ameunda kamati ya ushindi ya timu ya Taifa (Taifa Stars) ambayo mwenyekiti wake ni Ghalib Said Mohammed (GSM) huku makamu mwenyekiti akiwa ni Salim Abdallah na Katibu wake ni Mhandisi Hersi Said.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TFF mapema leo, wajumbe wa Kamati hiyo watakuwa Haji Manara, Patrick Kahemele, Jerry Muro Pamoja na Abdallah Bin Kleb.

Kamati hiyo itasaidia kuipa motisha timu ya Taifa ya Tanzania kuweza kushinda katika michuano yake ya kirafiki na timu nyingine za kitaifa.

banner

Taifa Stars ilipokea Kichapo katika mchezo wa kirafiki juzi,Octoba 11, ambapo Burundi ilijipatia ushindi wa bao 1-0 ikiwa ugenini.

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited