Home Makala Tiboroha Mkurugenzi mpya wa mpira Azam Fc

Tiboroha Mkurugenzi mpya wa mpira Azam Fc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya soka ya Azam Fc leo hii wamemtambulisha Katibu Mkuu wa zamani wa klabu ya soka ya Yanga Dokta Jonas Tiboroha kuwa mkuugenzi mpya wa mpira wa klabu hiyo.

Tiboroha ametambulishwa na Mtendaji mkuu wa klabu hiyo  Abdulkarim Nurdin Popat kushika wazifa huo mbele ya waandishi wa habari.

Mkurugenzi huyo mpya atakuwa na kazi ya kuboresha idara na muundo mzima wa mpira wa miguu wa Azam Fc kuanzia timu za vijana,wakubwa,benchi la ufundi pamoja na maswala yote ya usajili.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited