Site icon Sports Leo

TPLB Waomba Radhi Kwa Kuisahau Yanga

Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Tanzania Stiven Mguto ameomba radhi wadau wa soka kwa kitendo cha kuisahau timu ya Yanga katika upangaji ratiba wa michezo ya ligi kuu wiki hii.

Timu zingine zimecheza katikati mwa wiki  huku Yanga ikiachwa wakati ina viporo vingi kuliko timu zingine.

“Ukikosea unasema nini? Samahani! Basi tunaomba tusamehewe kama binadamu tunakosea, lakini wakitaka kutumia kama fimbo kutuadhibu sawa”alisema Mguto.

Exit mobile version