Home Makala United Wampata Mbadala Wa Rashford

United Wampata Mbadala Wa Rashford

by Sports Leo
0 comments

Manchester United imekamilisha dili la kumpata  Odion Ighalo kwa mkopo wa  pauni milioni tatu ingawa dili la United kumnunua jumla halijakamika.

Odion Ighalo anakuwa mbadala wa Marcus Rashford ambaye ndiye kinara wa United akiwa na mabao 14 ila kwa sasa anasumbuliwa na majeruhi ambayo yatampelekea kukaa nje ya uwanja kwa muda wa miezi sita.

Vita kubwa wamepata United kuwania  saini ya mchezaji huyo kwani Jose Mourinho wa Spurs  naye alikuwa anamuhitaji Ighalo kabla dirisha la mwezi Januari halijafugwa.

banner

Nyota huyoanatarajiwa kutua  United mwishoni mwa msimu huu akiwa chini ya Ole Gunnar Solskjaer ambaye amesema kuwa Odion ni mchezaji mwenye uzoefu na uwezo ndani ya Uwanja.

Nyota huyo raia wa Nigeria, mwenye miaka 30 amefunga jumla ya mabao 46 kwenye mechi 72 alizocheza akiwa na Shanghai Shenhua.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited