Home Makala Wanne Stars kuikosa Benin

Wanne Stars kuikosa Benin

by Sports Leo
0 comments

Wachezaji wanne wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ wataukosa mchezo wa Alhamisi dhidi ya Benin kuwania tiketi ya kufuzu michuano ya kombe la dunia Qatar 2022 kutokana na sababu mbali.

Wachezaji hao ni mabeki Erasto Nyoni,Bakari Mwamnyeto,Shomari Kapombe na kiungo Jonas Mkude.

Mwamyeto na Kapombe wataukosa mchezo huo kutokana na majeraha waliyopata hivi karibuni wakivitumikia vilabu vyao huku Erasto Nyoni sababu ikiwa haiko wazi japo inasemekana naye ni matatizo ya kiafya.

banner

Maswali mengi ya wadau wa soka nchini yamekuwa ni kwa kiungo Jonas Mkude ambaye taarifa kutoka kwa Meneja wa Taifa Stars Nadir Haroub mchezaji huyo aliomba ruhusa na kuruhusiwa kutokana na sababu za kifamilia,lakini cha kushangaza ni kuonekana kwake kwenye mazoezi ya klabu yake ya Simba huko Bunju.

Tetesi zinadai kuwa mchezaji huyo ameondolewa Stars kutokana na sababu za kinidhamu japo hazijaanishwa ni zipi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited