Home Makala Yanga Kumlipia Morrison Cas

Yanga Kumlipia Morrison Cas

by Sports Leo
0 comments

Makamu Mwenyekiti wa Yanga Fredrick Mwakalebela amekiri timu hiyo kudaiwa na wanaendelea kulipa madeni hayo ambayo mengi wameyarithi kutoka katika uongozi uliopita.

Jana kuliibuka taarifa kuwa Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhisi wa Michezo (CAS) imeiamuru klabu ya Yanga kumlipa dola 20,000 aliyekuwa mshambuliaji wake Amissi Tambwe ikiwa ni madai ya fedha za usajili na malimbikizo ya mishahara ya miezi mitatu

Mwakalebela amesema uongozi wao ulirithi madeni kutoka uongozi uliopita hivyo wanaendelea kuyalipa madeni hayo

banner

“Tumerithi vitu vingi yakiwemo madeni kutoka kwa uongozi uliopita, hata hili deni ya Tambwe ni miongoni mwa madeni hayo. Tunawahakikishia Wanayanga kuwa deni hili litalipwa,” alisema Mwakalebela

Aidha Mwakalebela aliongeza kuwa pia watalipia fedha walizotakiwa walipe ili kesi yao dhidi Bernard Morrison iweze kusikilizwa na CAS

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited