Home Makala Yanga sc Vs Mbao Fc Yahamishiwa Ccm Kirumba

Yanga sc Vs Mbao Fc Yahamishiwa Ccm Kirumba

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Yanga sc imeuhamisha mchezo wake wa kombe la shirikisho nchini la Azam Sports dhidi ya Mbao Fc kutoka uwanja wa Benjamin Mkapa mpaka uwanja wa Ccm Kirumba jijini Mwanza kufuatia uwanja wa Mkapa kuwa na matumizi mengine.

Awali mchezo huo ulipangwa kufanyika katika uwanja wa Mkapa siku ya Jumamosi Januari 29 lakini taarifa iliyotolewa na shirikisho la soka nchini imeonyesha kuhamishwa kwa mchezo huo mpaka jijini Mwanza huku muda wa mchezo ukibadirika kutoka saa moja usiku mpaka saa kumi jioni kutokana na uwanja huo kutokua na taa za kumulikia wakati wa usiku.

Yanga sc inatafuta ubingwa wa kombe hilo la shirikisho ambalo msimu uliopita ililikosa baada ya kufungwa mchezo wa fainali na Simba sc mkoani Kigoma.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited