Home Makala Yanga sc Wamuaga Magufuri

Yanga sc Wamuaga Magufuri

by Sports Leo
0 comments

UONGOZI wa klabu ya Yanga pamoja na kikosi chao leo Jumapili asubuhi wamekua miongonj mwa wananchi waliofika  katika msafara wa kumuaga aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Pombe Magufuli katika uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

Yanga jana Jumamosi jioni ilisimamisha kambi yao na kutoa fursa kwa wachezaji wao leo Jumapili kwenda kutoa heshima zao za mwisho kwa Rais huyo aliyeaga Dunia Machi 17 jioni baada ya kuugua ugonjwa wa moyo.

Wachezaji na viongozi wa klabu hiyo walikutana makao makuu ya klabu saa 3:00 asubuhi kisha ndio msafara wao ukaanza kwenda katika uwanja wa Uhuru.

banner

Kupitia katika ukurasa wao rasmi wa Instagram ulielezea kuwepo kwa tukio hilo kwa wachezaji na viongozi wao siku ya leo.
Shughuli za kuaga mwili wa marehemu Magufuli zilianza jana kwa kuongozwa na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, mawaziri, viongozi na kufuatiwa na wananchi wa kawaida.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited