Timu ya wananchi Yanga leo imemshusha Bongo Carraca Antonio Domingoz Pinto ambaye alikuwa mtendaji Mkuu wa klabu ya Ureno Benfica kwa miaka 10 ili kuanza kazi ya kushauri kueleka mabadiliko ya kimfumo ya uendeshaji wa klabu.
Nguli huyo wa mfumo wa soka la kisasa ameletwa kwa hisani kubwa ya kampuni ya Gsm ambao ni wadhamini wakubwa wa Yanga sc.
Carraca Antonio amepokelewa leo uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere na Makamu Mwenyekiti wa Yanga Fredrick Mwakalebela na Mkurugenzi wa Uwekezaji wa GSM Mhandisi Hersi Said.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.