Home Makala Yanga Yapindua Benchi La Ufundi

Yanga Yapindua Benchi La Ufundi

by Sports Leo
0 comments

Yanga Sc imeamua kuwaondoa wazawa wote katika benchi la ufundi na kubakiza raia wageni wawili kutoka Afrika Kusini mara baada ya kumpiga chini kocha mkuu,Luc Eymael kwa tuhuma za ubaguzi.

Mwenyekiti wa kamati ya ufundi wa Yanga,Dominick Albinius amesema kuwa baada ya kuwaondoa wachezaji wao 14 sasa wamefanya mabadiliko pia katika benchi la ufundi.

Aliongeza kwa kusema kuwa aliyekuwa kocha wao msaidizi wa kwanza,Charles Mkwasa amemaliza muda wake hivyo anahitaji kupumzika sambamba na kocha wa makipa ,Peter Manyika huku aliyekuwa meneja wa kikosi,Abeid Mziba na mtunza vifaa,Fred Mbuna wao wamebadilishiwa majukumu.

banner

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited