Home Masumbwi Dulla Mbabe apigwa na Mkongo

Dulla Mbabe apigwa na Mkongo

by Sports Leo
0 comments

Bondia wa Tanzania Abdallah Pazi maarufu kama Dulla Mbabe amepigwa katika pambano la uzito wa kati lililopewa jina la ‘Kiboko ya Wageni’ usiku wa kuamkia dhidi ya Tshimanga Katompa kutoka Congo.

Katika pambano hilo la raundi 10 lililofanyika katika ukumbi wa TPA Sabasaba Jijini Dar es salaam lilishuhudia Dulla akipigwa kwa pointi katika pambano hilo la kusisimua huku ngumi zikipigwa kwelikweli.

Katompa ambaye ambaye ameshinda mapambano yake yote kwa KO alionekana kumfahamu vizuri mpinzani wake huyo kwani alionekana kutawala vizuri mchezo huo licha ya uwepo wa mashabiki wa Dulla Mbabe ukumbini hapo.

banner

Hili ni pambano la pili mfululizo kwa Dulla kupoteza baada ya lile na mpinzani wake wa jadi Twaha Kiduku huku maswali yakiibuka juu ya nini hatma ya mwanamasumbwi huyo ambaye ameanza kupoteza mvuto kwa wapenzi wa ngumi nchini.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited