Home Masumbwi Mwakinyo kutetea ubingwa dhidi ya Mmalawi

Mwakinyo kutetea ubingwa dhidi ya Mmalawi

by Sports Leo
0 comments

Bondia Mtanzania ambaye pia ni bingwa wa Afrika Hassan Mwakinyo anatarajia kupanda ulingoni usiku wa leo katika pambano la kimataifa la kutetea mkanda wa Africa Boxing Union (ABU) kwa uzito wa light middleweight dhidi ya Mmalawi Julius Indongo.

Pambano hilo litafanyika hapa nchini katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es salaam ambalo litakuwa ni la raundi 12 na litarushwa hewani na kituo cha azam media.

Indongo anayeishi Marekani mpaka sasa amekwishapigana mapambano 23 proffesional akipoteza mapambano matatu tu huku akishinda 12 kwa knockout,pia amewahi kuwa bingwa wa WBO upande wa Afrika.

banner

Katika hatua nyingine bondia mwingine kutoka Tanzania Tony Rashid naye atapambana ulingoni kutetea ubingwa wa African Boxing Union Super Bantam title dhidi ya Bongani Mahlangu wa Afrika Kusini katika pambano la raundi 12.

Mapambano mengine ya utangulizi yanatarajiwa kuanza mida ya saa kumi na mbili jioni.

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited