Bondia Deontay Wilder ametemana na kocha wake Mark Breland baada ya kupoteza pambano lake dhidi ya Muingereza Tyson Fury siku ya Jumapili Asubuhi.
Bondia huyo alipigwa kwa TKO raundi ya saba baada ya kocha wake kurusha taulo ulingoni kuashiria kukubali kipigo hicho cha bondia huyo Mmarekani na hicho ndicho kilichosababisha kuachana na kocha huyo.
Pia nyota huyo amezungumzia mavazi aliyovaa kama moja ya sababu ya yeye kupigwa “Hakuniumiza hata kidogo, lakini ukweli rahisi ni kwamba sare zangu ndio zilikuwa nzito sana kwangu,” Wilder alimwambia Yahoo Sports. “Sikuwa na nguvu miguuni tangu mwanzoni mwa pambano. Katika mzunguko wa tatu, miguu yangu ilipigwa kama na butwa hivi. Lakini mimi ni shujaa na watu wanajua kuwa mimi ni shujaa. ”
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.