Home Soka Ahmed Musa Agoma Kupanda Basi

Ahmed Musa Agoma Kupanda Basi

by Dennis Msotwa
0 comments

Nyota mpya wa Kano Pillars ya Nigeria Ahmed Musa (28) amegoma kusafiri na klabu kwenda mikoani bila usafiri wa ndege akidai kusafiri kwa basi umbali mrefu sio salama kwake. Nyota huyo wa zamani wa Leicester City atacheza mechi za nyumbani tu.

Musa aliyewika katika ligi kuu nchini Uingereza alijiunga na timu hiyo kama mchezaji huru lakini ametoa masharti ya kucheza mechi za nyumbani tu katika uwanja wa Sani Abacha huku pia atacheza zile za karibu ikiwa watamhakikishia usalama wake huku akihitaji usafiri wa ndege kwa mechi za mbali.

Staa huyo kutokana na masharti hayo atakosa michezo dhidi ya Warri Wolves na Plateau United kutokana na kutokuwapo kwa usafiri wa ndege huku uongozi wa klabu hiyo ukikubalina na wazo la nyota huyo ambaye aliitumikia timu hiyo wakati anaanza soka kati ya 2009 mpaka 2012.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited