Home Soka Alliance Wapaa Kenya

Alliance Wapaa Kenya

by Sports Leo
0 comments

Timu ya soka ya Alliance Fc imeondoka jijini Mwanza kwenda nchini Kenya kwa mwaliko maalumu wa kucheza mechi za kirafiki kujiweka sawa na ligi kuu inayoendelea nchini ambapo imesimama kupisha michuano ya kimataifa ya kalenda ya Fifa.

Ukizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza leo uongozi wa timu hiyo umesema safari hiyo ni mwaliko maalumu wa timu ya Gormahi Fc ambayo imeialika timu hiyo kushiriki mchezo huo huku ikiwaahidi kuwatafutia michezo mingine ya kirafiki ili kujiweka fiti zaidi.

Safari hiyo ya pia imewezeshwa na benki ya Access Bank ambao ni moja ya wadhamini wa klabu hiyo huku wadhamini wengine wakiwa ni kampuni ya Emirate Alluminium Profile.

banner

Alliance inakabiliwa na mechi ngumu ya ligi kuu Tanzania bara dhidi ya Yanga sc baada ya mapumziko ya michuano ya kimataifa yatakapomalizika.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited