Home Soka Ancelloti Atimuliwa Napoli

Ancelloti Atimuliwa Napoli

by Sports Leo
0 comments

Licha ya kuiongoza Napoli kuibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Genk na kufuzu hatua ya mtoano timu ya Napoli imemtimua kocha huyo saa moja baada ya mechi hiyo.

Kocha huyo mwenye miaka 60 ametimuliwa baada ya mechi hiyo kufuatia kutokua na mwenendo mzuri kwenye ligi akipata ushindi mara moja kwenye mechi kumi na kuiweka timu hiyo nafasi ya saba kwenye msimamo wa ligi kuu nchini Italia (Serie A).

Inasemekana Napoli inaweza kumuajiri Gennaro Gattuso kuchukua nafasi hiyo ya Carlo Ancelloti huku wadau wa michezo wakimhusisha na kurudi ligi ya Uingereza miaka nane tangu atimuliwe na Chelsea licha ya kuipa kombe.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited