Home Soka Azam Fc Ugonjwa Ule Ule

Azam Fc Ugonjwa Ule Ule

by Sports Leo
0 comments

Licha ya kumtimua Kocha Arstica Cioaba klabu ya Azam Fc bado imeendelea na wimbi la kuwa na matokeo mabovu katika michezo ya ligi kuu nchini baada ya leo kulazimishwa sare ya 1-1 na Biashara United katika uwanja wa Karume mkoani Mara.

Ayoub Lyanga aliipa Azam Fc uongozi dakika ya 20 lakini bao hilo lilisawazishwa na Thomas Omwenga dakika ya 58 kwa shuti kali na kumshinda kipa David Mapigano.

Biashara inabidi wajilaumu wenye baada ya kukosa penati baada ya mchezaji wao kufanyiwa madhambi ndani ya eneo la mita 18 lakini mpigaji alikosa penati hiyo baada ya kupiga nje.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited