Matajiri wa Dar es salaam Azam FC wametambulisha basi jipya litakalokuwa kinatumiwa na timu ya wakubwa ya wanaume ya soka ya klabu hiyo yenye makazi yake Chamazi nje kidogo ya jiji la Dar es salaam.
Utambulisho huo umefanyika kupitia ukurasa wao wa instagram wakitumia picha mbalimbali za muonekano wa basi hilo zikiambatana na ujumben” Here wa go,Ndege ya ardhini,Marcedez Benz irizar i6S plus.
Azam hawajaanza vizuri kwenye ligi kuu soka Tanzania Bara msimu huu kwa kukusanya alama moja tu katika michezo miwili ya ligi hiyo,lakini wameendeelea kujiimarisha nje ya uwanja kwa kuifanya klabu kuwa na hadhi ya kimataifa kwa kufanya uwekezaji mkubwa wa miundombinu mbalimbali.