Mechi kati ya Azam Fc na Namungo Fc imemalizika kwa sare baada ya dakika 90 za mchezo uliofanyika katika uwanja wa Chamazi jijini Dar es salaaam.
Mabao ya Azam Fc yalifungwa na Idd Nado dakika za 19 na 74 huku Namungo wakifunga kupitia kwa Charles Manyama dakika ya 25 huku Stephen Sey akifunga bao la kusawazisha dakika za mwisho mwa mchezo.
Sare hiyo inamaanisha kwamba Azam Fc imeshindwa kupata ushindi katika mechi tano mfululizo na kuzidi kuacha pengo la alama kwa Yanga sc wenye alama 34 huku Azam Fc wakiwa na alama 27.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.