Klabu ya Azam fc imeibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya timu ya biashara united katika mchezo uliofanyika katika uwanja wa Chamazi unaomilikiwa na klabu hiyo.
Iliwachukua Azam Fc dakika mbili kuandika bao la kwanza lililofungwa na Idd Nado kabla ya kuongeza bao jingine lililofungwa na Nicolas Wadada dakika ya 21 huku wageni wakipata bao la kufutia machozi dakika 32 Innocent Edwin.