Home Soka BAADA YA ULAYA, SAMATTA ATANGAZA KUREJEA SIMBA

BAADA YA ULAYA, SAMATTA ATANGAZA KUREJEA SIMBA

by Sports Leo
0 comments


Straika tegemo katika timu ya KRC Genk inayoshiriki Ligi Kuu Ubelgiji, Mbwana Samatta, amesema kuwa endapo atamaliza harakati za maisha yake ya soka atarejea Tanzania kuungana na Simba.
"Wachezaji wengi wakubwa wanapokaribia kustaafu soka hurudi kwenye klabu zao vya zamani ambavyo viliwatoa.
"Nilikuwa mchezaji wa Simba zamani, hata nitakaporudi baadaye nafikiri nafasi ya kwanza itakuwa kwa Simba kwa sababu niliwahi kuitumikia lakini kama watakuwa hawanitaki ndio nitaangalia sehemu nyingine.
.
"Kwa heshima yao kwa sababu niliwahi kuwa mchezaji wao kwa hiyo nafasi ya kwanza lazima itakuwa kwao."
TP Mazembe ya DR Congo ilimsajili Samatta akitokea Simba na alicheza kwa mafanikio makubwa na kuwapa ubingwa wa Afrika.
Baada ya hapo alianzisha safari maya ya maisha alipojiunga na KRC Genk ambayo pia amefanikiwa kuipa ubingwa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited