Home Soka Bado Tatu Tu

Bado Tatu Tu

by Dennis Msotwa
0 comments

Baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Mbeya City Fc sasa klabu ya Simba sc inahitaji alama tatu tu ili kutwaa taji la ligi kuu Tanzania bara kwa mara ya nne mfululizo.

Endapo klabu hiyo itafikisha alama hizo itakua imetwaa taji hilo baada ya kujihakikishia kwamba hakuna timu ambayo itazifikia alama hizo huku ikiwa tayari Azam Fc waliokatika nafasi ya tatu wakiwa wamekosa uwezekano wa kuwa mabingwa baada ya Simba sc kufikisha alama 73 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yeyote isipokua Yanga sc.

Mchezo unaofata wa ligi kuu utakua baina ya timu hizo zilizopo nafasi ya juu ya msimamo na endapo Yanga sc watafungwa basi Simba sc watatawazwa mabingwa kupitia mchezo huo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited