Home Soka Bado Yupo Sana

Bado Yupo Sana

by Sports Leo
0 comments

Rais wa klabu ya Barcelona Jose Bartomeu amesema kuwa anaamini kuwa mshambuliaji wake Lionel Messi kuwa ataongeza mkataba wa mwaka moja licha ya kuhusishwa kutimka klabuni hapo.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 33 amekuwa anahusishwa kuondoka ndani ya klabu hiyo ya Barcelona hasa baada ya kutokua na msimu mzuri pamoja na kuwa na migongano na viongozi wa klabu hiyo mara kadhaa hasa kuhusu uendeshaji wa timu.

Messi alihusishwa kuondoka baada ya kutokubaliana na mbinu za kocha wa timu hiyo Quique Satien juu ya ufundishaji wa timu hiyo pia aliwahi kukwaruzana na mkurugenzi Erick Abidal.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited