Home Soka Barca Waipisha Madrid Kileleni

Barca Waipisha Madrid Kileleni

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Barcelona imeshushwa katika msimamo wa ligi kuu nchini Hispania baada ya jana kushindwa kuibuka na ushindi dhidi ya Atletico Madrid baada ya kulazimishwa sare ya mabao 2-2.

Barca walifaidika na kitendo cha kutokua makini kwa Diego Costa ambaye alijifunga dakika ya 11 japo makosa yake yalifutwa na Saul Niguez aliyefunga kwa penati dakika ya 19 huku Messi akifanikiwa kufunga bao la pili kwa Barca na la 700 kwake katika michuano yote dakika ya 50 japo nalo halikudumu ambapo Saul Niguez alifunga penati ya pili dakika ya 62.

Kwa matokeo hayo Real Madrid wameendelea kusalia kileleni licha ya kuwa na mchezo mmoja mkononi wakiwa na pointi 71 huku Barca wakiwa na pointi 70 katika nafasi ya pili.

banner

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited