Home Soka Bayern Mziki Mnene

Bayern Mziki Mnene

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Bayern Munich imefanikiwa kuifikia rekodi ya Fc Barcelona ya kuvuna makombe sita kwa msimu mmoja baada ya jana kufanikiwa kuifunga timu ya Tigres katika mchezo wa fainali ya klabu bingwa duniani katika mchezo uliofanyika nchini Qatar.

Bao pekee la Benjamin Pavard liliihakikishia Bayern taji la sita ndani ya miezi sita huku mastaa mbalimbali wa timu hiyo wakitwaa tuzo binafsi.

Kutwaa kwa taji hilo kumeifanya timu hiyo kuifikia rekodi iliyowekwa na Barcelona mwaka 2009 huku pia likiwa ni taji la sita kwa kocha wa klabu hiyo Hans Flick tangu aanze kuifundisha timu hiyo mwezi novemba 2019.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited