Home Soka Benzema Aiondosha Psg

Benzema Aiondosha Psg

by Dennis Msotwa
0 comments

Mabao matatu ya mshambuliaji wa klabu ya Real Madrid Karim Benzema yalitosha kuwaondosha Psg katika mchezo wa hatua ya 16 bora ya michuano ya klabu bingwa barani ulaya mchezo uliofanyika jijini Madrid.

Paris st.German wakiwa mbele kwa bao 1 waliloshinda katika mechi ya awali jijini Paris walihitaji sare ya aina yeyote kuweza kufuzu hatua ya robo fainali lakini ndoto hizo ziliyeyuka kipindi cha pili baada ya Benzema kufunga mabao matatu kipindi na kuwatoa Psg katika michuano hiyo licha ya kutangulia kufunga dakika ya 39 kupitia kwa Kylian Mbappe.

Mshambuliaji huyo mkongwe Mfaransa, Karim Benzema alifunga katika  dakika za 61,76 na 78 baada ya PSG kutangulia kwa bao la mshambuliaji Mfaransa mwenzake na kuzua shangwe kwa mashabiki wa Real Madrid uwanjani hapo.

banner

Kutokana na ushindi huo Real Madrid wanasonga mbele kwa ushindi wa jumla wa 3-2, kufuatia kufungwa 1-0 kwenye mchezo wa kwanza wa 16 Bora Ufaransa kwa  bao la Mbappe.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited