Home Soka Boko,Ajibu Waimaliza KMC

Boko,Ajibu Waimaliza KMC

by Dennis Msotwa
0 comments

Timu ya Simba sc leo imeibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya timu ya manispaa ya Kinondoni(Kmc) katika mchezo wa kirafiki uliofanyika katika uwanja wa Mo Simba Arena bunju jijini Dar es salaam.

Katika mchezo huo wenye lengo la kujiandaa na ligi kuu Tanzania bara Kmc ilikua ya kwanza kupata bao dakika ya 32 kupitia kwa Charles Ilanfya lakini bao hilo halikudumu baada ya Simba kusawazisha kupitia kwa John Boko aliyefunga bao jingine dakika ya 73 kabla ya Ibrahim Ajib kufunga bao la mwisho dakika ya 88.

Simba hivi leo imecheza michezo miwili ya kirafiki ambapo asubuhi iliilaza Transit Camp mabao 4-2 na jioni kushinda mabao 3-1 dhidi ya KMC.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited