Afisa Habari-Yanga Hassan Bumbuli ameshinda rufaa ya kufungiwa kujihusisha na masuala ya soka kwa miaka mitatu hukumu ambayo ilitolewa na TFF ikielezwa Bumbuli amekaidi uamuzi wa Kamati ya Maadili dhidi yake.
Taarifa za kushinda kwa rufaa ya Afisa huyo zimesambaa hivi leo katika mitandao mbalimbali huku bado taarifa rasmi kutoka shirikisho la soka nchini TFF ikiwa bado haijatoka.
Kwa maana hiyo, Bumbuli yupo huru kuendelea na shughuli za soka ikiwa ni pamoja na kuitumikia klabu yake ya Yanga.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.