Home Soka Buriani Magufuri,Michezo Yasimama

Buriani Magufuri,Michezo Yasimama

by Dennis Msotwa
0 comments

Shirikisho la soka nchini Tanzania Tff limesimamisha shughuli zote za michezo ya soka nchini kufuatia kifo cha Rais John Pombe Magufuli kilichotokea jana jioni kufuatia kusumbuliwa na maradhi ya moyo.

Awali baada ya taarifa kusambaa kufuatia kutoonekana hadharani kwa muda mrefu huku shughuli zikiendelea kama ilivyo kawaida lakini kufuatia tangazo rasmi la serikali kuhusu msiba huo kumesababisha shughuli za michezo ya soka kusimamishwa na shirikisho hilo.

Moja ya ratiba iliyoathirika ni mechi ya kirafiki baina ya timu ya taifa ya Tanzania iliyokua icheze mchezo wa kirafiki dhidi ya Kenya machi 18,ratiba hiyo imeahirishwa japo timu hiyo itaendelea kuweka kambi nchini Kenya.

banner

Taarifa rasmi kutoka Tff inaonyesha kuwa michezo mbalimbali ya soka itasimama kwa muda wa wiki mbili kupisha kipindi cha maombolezo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited