Home Soka CAS yapeleka tena mbele kesi ya Morrison

CAS yapeleka tena mbele kesi ya Morrison

by Sports Leo
0 comments

Mahakamma ya usuluhishi wa michezo duniani (CAS) imesogeza kesi ya kimkataba kati ya klabu ya Yanga na mchezaji wa Simba SC Benard Morrison kutoka leo Septemba 21 hadi Oktoba 26 mwaka huu.

Morrison anatuhumiwa na Yanga SC kujiunga kwa watani wao wa jadi Simba SC wakati akiwa bado ana mkataba na mabingwa hao wa kihstoria.

Awali kesi yake ilitarajiwa kuwa ingetolewa maamuzi baada ya kusikilizwa na CAS kwa njia ya video Julai mwaka huu na hukumu yake wakisema ingetolewa kufikia August 24.Ilipofika August 24 CAS waliomba radhi kwa Yanga na Morrison kuwa walijisahau hivyo watalishughulikia swala hilo na kutoa hukumu Septemba 21 mwaka huu.

banner

Wadau na wapenzi wa soka walikua wakisubiria hukumu ya kesi hiyo kwa hamu siku ya leo kabla ya CAS kupitia tovuti yake kueleza kuwa hukumu ya kesi hiyo imesogezwa hadi Oktoba 26 mwaka huu.

Morrison alishinda kesi hiyo hapa nchini kupitia kamati ya hadhi na maadilim ya wachezaji ya TFF lakini Yanga SC hawakuridhika na kuamua kukata rufaa CAS ambapo kesi imeshasikilizwa kilichobaki ni hukumu tu kujua mbivu na mbichi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited