Mabingwa wa klabu bingwa Ulaya Chelsea wamefanikiwa kuchukua kombe la Uefa super cup baada ya kuwafunga manyambizi wa njano klabu ya soka ya Villareal kutoka Hispania kwa changamoto ya mikwaju ya penati 7-6.
Timu hizo zilitoka sare ya goli 1-1 ndani ya dakika na kupelekea mchezo kwenda dakika 30 za nyongeza ambapo pia matokeo yalikuwa suluhu ya 0-0.
Chelsea ilijipatia goli lake kunako dakika ya 27 kupitia Hakim Ziyech akimalizia pasi ya Kai Havertz,huku Villareal ikisawazisha dakika ya 81 kupitia kwa Gerard Moreno.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Golikipa wa Chelsea Kepa Arrizabalaga akiokoa mikwaju miwili ya penati na kuipa ushindi timu yake.