Home Soka Chelsea mabingwa Uefa Super Cup

Chelsea mabingwa Uefa Super Cup

by Sports Leo
0 comments

Mabingwa wa klabu bingwa Ulaya Chelsea wamefanikiwa kuchukua kombe la Uefa super cup baada ya kuwafunga manyambizi wa njano klabu ya soka ya Villareal kutoka Hispania kwa changamoto ya mikwaju ya penati 7-6.

Timu hizo zilitoka sare ya goli 1-1 ndani ya dakika na kupelekea mchezo kwenda dakika 30 za nyongeza ambapo pia matokeo yalikuwa suluhu ya 0-0.

Chelsea ilijipatia goli lake kunako dakika ya 27 kupitia Hakim Ziyech akimalizia pasi ya Kai Havertz,huku Villareal ikisawazisha dakika ya 81 kupitia kwa Gerard Moreno.

banner

Golikipa wa Chelsea Kepa Arrizabalaga akiokoa mikwaju miwili ya penati na kuipa ushindi timu yake.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited