Home Soka Chelsea Yaipiga Juventus 4-0

Chelsea Yaipiga Juventus 4-0

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Chelsea imefanikiwa kuifunga Juventus Fc mabao 4-0 katika mchezo wa michuano ya klabu bingwa barani ulaya(Uefa) uliofanyika katika uwanja wa Stamford Bridge huku timu hiyo ikfanikiwa kuonyesha kiwango kizuri katika dakika zote za mchezo huo.

Trevo Chalobah aliifanya Chelsea kwenda mapumziko ikiwa mbele kwa bao 1 baada ya kufunga bao hilo dakika ya 25 huku Reece James akiongea wenyeji bao la pili dakika kumi baada ya kipindi cha pili kuanza na Callum Hudson-Odoi aliongeza bao la tatu dakika tatu baadae huku dakika za mwishoni za nyongeza Timo Warner aliongeza bao la 4 na kuifanya timu hiyo kufuzu hatua ya mtoano ikiwa na alama 12.

Ushindi huo wa Chelsea umehitimisha safari ya Zenit na Malmo katika kundi H ndani ya michuano hiyo baada ya kuwa na alama ndogo huku Juventus wakiungana na Chelsea hatua ya Mtoano.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited