Home Soka CONTE kutua SPURS

CONTE kutua SPURS

by Sports Leo
0 comments

Kocha wa zamani wa vilabu vya Juventus,Chelsea na Inter Milan Antonio Conte amefikia makubaliano ya msingi na klabu ya Tottenham Hotspurs kuwa mkufunzi wa timum hiyo ya Kaskazini mwa London.

Conte atasaini mkataba na klabu hiyo leo Jumanne utakaomuweka Spurs hadi mwaka 2023.

Mkurugenzi wa michezo Fabio Paratici alimhitaji Conte tangu mwezi Julai lakini walishindwana dakika za mwisho na kutua kwa Mreno Nuno Santo ambaye amefutwa kazi.

banner

Muitaliano huyo sio muumini wa kuchukua timu katikati ya msimu na alikuwa tayari kubadili mawazo yake alipokaribia kupata ofa ya Man Utd kabla ya kuamua kubakia na kocha wao Ole Solskjaer.

Conte alishawahi kufanya kazi na Fabio Paratici katika klabu ya Juventus na ndiye aliyemshawishi kuukubali mradi wa Totenham,kocha huyo amehakikishiwa kupewa sapoti katika madirisha yajayo ya usajili kukiboresha kikosi hicho.

Ujio wa mkufunzi huyo mshindi wa mataji mbalimbali huenda ukamshawishi nahodha wa klabu hiyo Harry Kane kusalia kwenye timu hiyo.conte

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited