Home Soka Corona Yasimamisha Serie A

Corona Yasimamisha Serie A

by Sports Leo
0 comments

Baadhi ya mechi ambazo zilitakiwa kupigwa leo nchini Italia zimehairishwa kutokana na hofu juu ya Virusi vya Corona ambavyo vinasambaa kwa kasi duniani.

Taarifa kutoka ESPN zinasema kwamba mechi ambazo zilitakiwa kupigwa katika mikoa ya kaskazini Lombardy na Veneto , kati ya Inter Milan dhidi ya Sampdoria, Sassuolo dhidi ya Atalanta na Hellas Verona dhidi ya Cagliari zote zimehairishwa .

ESPN wameripoti kwamba miji mingi katika ukanda wa Kaskazini mwa Italia imefungwa baada ya vifo vya watu wawili walioathirika na Virusi vya Corona .

banner

Ugonjwa huo ulianzia nchini china na unadaiwa usambaa baadhi ya nchi duniani ambapo mpaka sasa inasemekana zaidi ya watu 1000 wamefariki nchini China Pekee.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited