Home Soka Corona Yasimamisha Serie A

Corona Yasimamisha Serie A

by Sports Leo
0 comments

Waziri mkuu wa Italia Guissepe Conte amesema michezo yote ya ligi kuu ya Italia maarufu kama Serie A itasimama mpaka April 3 ili kupisha maambukizi ya virusi vya ugonjwa wa Corona ulioingia nchini humo.

Waziri huyo amefikia maamuzi hayo baada ya takribani watu 450 kuripotiwa kupoteza maisha huku zaidi ya watu 9000 inakadiliwa wameambukizwa ugonjwa huo unaoenezwa kwa njia yan hewa na majimaji ya mwilini.

Awali serikali nchini Italia ilizuia mikusanyiko ya watu ikiwemo kuamuru mechi za ligi zichezwe bila mashabiki ikiwemo mechi iliyochezwa wiki iliyoisha baina ya Intermilan dhidi ya Juventus ambapo hakukua na mashabiki walioingia uwanjani.

banner

Licha ya kusimamishwa kwa ligi hiyo,michuano ya kimataifa ikiwemo klabu bingwa barani ulaya na ligi ya kombe la Europa itaendelea kama kawaida bila mashabiki.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited