Home Soka Enrique Arejea Spain

Enrique Arejea Spain

by Sports Leo
0 comments

Luis Enrique ameteuliwa kocha mpya wa timu ya taifa ya Hispania baada ya hapo awali kujiengua kutokana na matatizo ya kiafya ya mwanaye wa kike.

Kocha huyo wa zamani wa Barcelona alijiuzulu mwezi june mwaka huu kutokana na afya ya mwanaye kutetereka baada ya kuugua kansa na baadaye alipoteza maisha mwezi septemba huku nafasi yake timu ya taifa ikichukuliwa na Roberto Moreno.

Erique atakua na kazi ya kuiandaa timu ili kufuzu michuano ya ulaya ya mwaka 2020 huku uzoefu wa kuinoa Barcelona kwa misimu mitatu ikitajwa kuwa chachu ya kupewa nafasi hiyo.

banner

Kabla ya nafasi hiyo Erique alikua anahusishwa kutua klabu ya Arsenal kuchukua nafasi ya Unai Emiry ambaye nafasi yake ipo matatani kufuatia mfululizo wa matokeo yasiyoridhisha

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited