Home Soka FIFA yaanza uchunguzi madai ya Afrika Kusini

FIFA yaanza uchunguzi madai ya Afrika Kusini

by Dennis Msotwa
0 comments

Shirikisho la mpira wa miguu duniani(FIFA) limefungua rasmi uchunguzi wa wazi juu ya madai ya timu ya Taifa ya Afrika Kusini juu ya penati ya utata waliyopewa Ghana katika mchezo wa kufuzu hatua za mtoano kutinga kombe la dunia Qatar 2022.

Chama cha soka Afrika Kusini kilituma kilituma barua ya malalamiko juu ya mwamuzi Maguette Ndiaye aliyewzawadia penati Ghana na kuwapa goli pekee la mchezo lililowawezesha kutinga hatua ya kumi bora.

Baada ya kupokea malalamiko hayo FIFA imeyajubali na kuanza uchunguzi mara moja.

banner

Katika mchezo huo mchezaji wa Ghana Daniel Amartey alijiangusha ndani ya eneo la kumi na nane wakati wa kugomea mpira wa kona dakika ya 33,hata hivyo mgusano kati yake na beki Rushine de Reuck ulikua ni mdogo sana ambao kikanua za soka haukupaswa kuwa ni adhabu.

Endapo FIFA wakijiridhisha baada ya uchunguzi kuwa ni kweli maamuzi ya mwamuzi Ndiaye yalikuwa na utata basi kuna uwezekano mkubwa mchezo huo kurudiwa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited