Home Soka Fiston Atimka Yanga sc

Fiston Atimka Yanga sc

by Dennis Msotwa
0 comments

Mshambuliaji wa klabu ya Yanga, Fiston Abdoul Razack, ametimka klabuni baada ya mkataba wake wa miezi sita kumalizika Julai 12, 2021 na huku kukiwa hakuna dalili za kuongezewa mkataba mpya.

mchezaji huyo alijiunga na Yanga sc chini ya kocha Cedrick Kaze mwezi januari mwaka huu kwa mkataba mfupi wa miezi sita tu,ameifungia Yanga bao moja Ligi Kuu Bara na bao lingine Kombe la FA ambapo Jumla ni mabao mawili katika michezo yote aliyocheza ya kimashindano na kirafiki.

Yanga sc haijaonyesha nia ya kuendelea na mshambuliaji huyo kutokana na kushindwa kulishawishi benchi la ufundi chini ya kocha Mohamed Nasredine Nabi.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited